Mkoa wa Zhejiang ulipata jina lake kutoka kwa Mto Zhe, kwa maana ya mto "usionyooka" au "uliopinda". Mito katika mkoa wa Zhejiang ina umuhimu kwa jamii kutoka kitambo, inatiririka kupitia miji ya zamani, kati ya nyumba za jadi zilizo na kuta nyeupe na paa nyeusi, na hunufaisha mashamba ya mpunga. Licha ya hayo, Zhejiang pia ni mojawapo ya mikoa Uchina ambayo ni tajiri zaidi na imeendelea zaidi, na maendeleo ya kasi yalibadili mkondo wa maji.

Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa linamutambua Waziri Mkuu wa India Narendra Modi kwa uungozi wake wa kishujaa kuhusiana na masuala ya mazingira katika ngazi ya kimataifa. Chini ya uongozi wa Narendra Modi, India iliahadi kukomesha matumizi ya plastiki zinazotumiwa tu mara moja katika nchi hiyo kufikia mwaka wa 2022. Waziri Mkuu, Modi, pia anaunga mkono na kupigania kuwepo kwa Muungano wa Kimataifa wa Nishati ya Jua, ambao ni ubia wa kimataifa wa kuimarisha matumizi ya nishati ya jua.

Joan Carling amekuwa akipigania haki za ardhi na za mazingira ya watu wa kiasili kwa zaidi ya miaka 20. Alishiriki kikamilifu katika Jukwaa la Mapatano la Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi na REDD+. Amefanya kazi kama Katibu Mkuu wa Mkataba wa Watu wa Asili ya Asia mara mbili. Pia alikuwa mwenyekiti wa Muungano wa Watu wa Cordillera.

Impossible Foods na Beyond Meat walishinda kwa pamoja Tuzo la Mabingwa wa Dunia, katika kitengo cha Sayansi na Ubunifu. Wanatoa vibadala vya kudumu kwa baga za nyama ya ng'ombe ambavyo ni rafiki zaidi kwa mazingira na vinatoa ushindani kwa ladha ya nyama. Washindi hawa wanaamini kuwa haiwezekani kufikia malengo ya Mkataba wa tabia nchi wa Paris bila kupunguza kilimo cha ufugaji kwa kiwango kikubwa.

Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron amelipa swala la utunzaji wa mazingira kipau mbele katika ajenda yake ya nchi za kigeni. Anatambuliwa kwa kupigania kuwepo kwa Muungano wa Kimataifa wa Nishati ya Jua na kukuza ushirikiano wa kimataifa ili kushughulikia masuala ya mazingira, na kwa uongozi wake kuhusiana na Mkataba wa Kimataifa wa Mazingira.