• 'Ant Forest', imepokea tuzo kuu la mazingira linatolewa na Umoja wa Mataifa katika kitengo cha motisha na kuchukua hatua
  • 'Ant Forest' walituzwa kwa kuwahimiza watumizi wa bidhaa kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa, hali iliyopelekea mradi mkubwa wa upandaji wa miti na sekta ya kibinafsi nchini China.

 

 

Septemba 19,  2019 -- 'Ant Forest', Mradi unaohimiza kutochafua mazingira, umeshinda tuzo la mwaka wa 2019 la Mabingwa wa Dunia. Tuzo hili la kiwango cha juu la mazingira linatolewa na Umoja wa Mataifa kutokana na juhudi zilizowezesha watu nusu bilioni walio na nia nzuri ya kupunguza hewa ya ukaa kupanda miti katika baadhi ya maeneo kame zaidi Uchina. 

 

Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa linatuza 'Ant Forest' katika kitengo cha 'Motisha na Kuchukua Hatua'.

 

Mradi uliozinduliwa na 'Ant Financial Services Group' hupendekeza matumizi ya nishati isiyochafua mazingira kwa kuwashawishi watumiaji wa bidhaa kupunguza hewa ya ukaa huku wanapoendelea na shughuli zao za kila siku ili kuyatunza mazingira. 

 

Watumizi wa 'Ant Forest' wanashauriwa kupunguza hewa ya ukaa kupitia shughuli zao za kila siku kama vile kutumia magari ya umma wanaposafiri na kulipia huduma mtandaoni. Kila wanapofanya hivyo, wanatuzwa alama za ‘green energy’ na zinapofikia idadi fulani, mti halisi hupandwa. Watumizi wanaweza kuona picha za miti yao kupitia setilaiti. Mbali na upandaji wa miti, watumizi wanaweza kuamua kutunza sehemu ya kipande cha ardhi kwenye jukwaa la 'Ant Forest', ambalo pia linatafuta kutumia ubunifu kupunguza umaskini na kuboresha maisha ya watu wanaokaa maeneo ya karibu na misitu hiyo kwa kutumia teknolojia ya kidijitali. 

 

Tangu kuzinduliwa kwake mnamo Agosti mwaka wa 2016, 'Ant Forest' na wabia kutoka katika mashirika yasiyokuwa ya serikali  (NGO), wamepanda takribani miti milioni 122 katika baadhi ya maeneo kame zaidi Uchina, ikiwa ni pamoja na maeneo kame ya Inner Mongolia, Gansu, Qinghai and Shanxi. Miti hiyo inapatikana katika eneo la hekta 112,000 (mu milioni 1.68);  Mradi huu ndio mkubwa sana Uchina wa upandaji wa miti unaofanywa na sekta za kibinafsi. 

 

"'Ant Forest'" ni idhibati ya jinsi teknolojia inavyoweza kubadili ulimwengu wetu kwa kutumia nishati nzuri na kuonyesha ubunifu wa watumizi kote ulimwenguni," alisema Inger Andersen, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa. 

 

“Ijapokuwa kuna changamoto kubwa zinazokabili mazingira, tuna teknolojia na maarifa ya kuzikabili na kubadili jinsi tunavyoishi katika sayari. Miradi kama  ya 'Ant Forest' ni mojawapo ya jinsi mwanadamu anavyoweza kutumia uerevu na ubunifu kuboresha maisha," alisema.

 

Haja ya kuchukua hatua kali kote ulimwenguli ili kukabiliana ya mabadiliko ya tabianchi itaangaziwa wakati wa Mkutano Mkuu wa Kushughulikia Mazingira ulioandaliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres’, utakaofanyika tarehe 23 Septemba mjini New York. Katibu Mkuu ametoa wito kwa viongozi duniani, wamiliki wa biashara na mashirika ya uraia kuhudhuria mkutano wakiwa na suluhisho tosha la jinsi watakavyopunguza uchafuzi wa hewa kwa asilimia 45 kufikia karne ijayo na kuepukana na hewa chafu kabisa kufikia mwaka wa 2050. Hii ni sambamba na Mkataba wa Paris kuhusu  tabianchi na Malengo ya Maendeleo Endelevu.  

 

Mkutano huu unalenga kutoa masuluhiho ya kipekee katika sekta za kipekee: kuhimiza matumizi ya nishati jadidifu duniani; miundo mbinu na miji endelevu na ya kudumu; mabadiliko ya kudumu ya  kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi; utengaji wa fedha na sekta za umma na za kibinafsi ili kuimarisha uchumi kwa kutochafua mazingira; na kilimo endelevu na utunzaji wa misitu na bahari.

 

Kutuzwa kwa 'Ant Forest' kama Bingwa wa Dunia inaonyesha umuhimu wa kutunza mifumo ya ekolojia ili kupunguza uzalishaji wa hewa inayosababisha mabadiliko ya tabianchi. Mnano Machi, Umoja wa Mataifa ulisisitiza umuhimu wa udharura wa kutunza mifumo inayowezesha maisha kwa kutangaza Karne ya kuanzia 2021 hadi 2030 kama karne ya Umoja wa Mataifa ya Kuboresha Mifumo ya Ekolojia. 

 

"Tuna furaha kubwa kupokea tuzo hili la Mabingwa wa Dunia," alisema Eric Jing, Mwenyekiti na Afisa Mkuu Mtendaji wa 'Ant Financial'. "'Alipay Ant Forest' ni ishara ya imani yetu kuwa teknolojia inaweza na ni sharti itumiwe kwa manufaa ya jamii. Tunashukuru watu wote wanaotumia teknolojia yetu na wabia ambao wametuwezesha kupanda miti milioni 122 na kukuza maono tunayoshiriki ya maendeleo endelevu ya kudumu. Kuvuma kwa 'Alipay Ant Forest' ni ishara kuwa umma uko tayari kuchukua hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Mabingwa wa Dunia, ni tuzo la kimataifa linalotolewa na Umoja wa Mataifa kwa heshima ya mazingira.  Lilianzishwa na Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) mwaka wa 2005 kuwatuza watu wa kipekee ambao matendo yao yamekuwa na athari chanya zinazoleta mabadiliko kwa mazingira.  Kutoka kwa viongozi duniani hadi kwa watetezi wa mazingira na hadi kwa wanaobuni teknolojia, waanzilishi hawa wanaoleta mabadiliko ili kutunza sayari yetu kwa ajili ya vizazi vijavyo hutuzwa.  

 

'Ant Forest' ni mojawapo wa washindi tano wa mwaka huu. Vitengo vingine ni pamoja na Uongozi wa Sera , Maono ya Ujasiriamali  na Sayansi na Ubunifu. Washindi wa mwaka wa 2019 watatuzwa wakati wa sherehe ya gala mjini New York tarehe 26 Septemba wakati wa kikao cha 74 cha Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa.  Wengine watakaotuzwa pia wakati wa hafla hii ni wanamazingira wa kipekee saba wa umri wa kati ya miaka 18 hadi miaka 30. Watatuzwa tuzo la Vijana Bingwa Duniani.

 

Watu waliowahi kushinda tuzo la Mabingwa wa Dunia ni Wachina waliobuni vitu na waleta mabadiliko, hasa katika nyanja ya kukabiliana na uchafuzi wa mazigira na majangwa.  Katika mwaka wa 2018 programu ya 'Green Rural Revival Programme' ilituzwa katika kitengo cha motisha na kuchukua hatua kutokana na kazi yake ya kusafisha maeneo ya maji yaliyochafuliwa na kuboresha ardhi iliyoharibika. Katika mwaka wa 2017, Jamii ya Upandaji Miti ya Saihanba ilituzwa katika kitengo cha motisha na kuchukua hatua kwa kufanya ardhi iliyoharibika Kusini mwa Inner Mongolia kuzalisha mimea mingi.  

 

MAKALA KWA WAHARIRI

 

Kuhusu Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa

Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa ni msemaji mkubwa wa kimataifa kuhusu mazingira. Hutoa uongozi na kuhimiza ushirikiano katika kutunza mazingira kupitia kuvutia, kuelimisha na kuwezesha mataifa na watu kuimarisha maisha yao bila kuhatarisha yale ya vizazi vijavyo.   

 

Kuhusu Weibo

Mabingwa wa Dunia huandaliwa kwa msaada wa ufadhili kutoka kwa  Weibo – Mtandao mkuu wa kijamii nchini China unaowezesha watu kuunda, kushiriki na kupata makala mtandaoni.  Weibo ina zaidi ya watumizi milioni 486 kila mwezi.

 

Kuhusu Mabingwa wa Dunia

Tuzo linalotelewa kila mwaka la Mabingwa wa Dunia  hutuza viongozi vya kipekee kutoka kwa serikali, mashirika ya uraia na sekta ya kibinafsi ambao matendo yao yamesababisha mabadiliko chanya kwa mazingira. Tangu mwaka wa 2005, tuzo la Mabingwa wa Dunia limewatuza washindi 88, kuanzia kwa wakuu wa nchi hadi kwa wanaobuni teknolojia.  

 

Kwa maelezo zaidi, tafadhali wasiliana na:

Keisha Rukikaire, UNEP Habari na Vyombo vya Habari, rukikaire@un.org, +254 722 677747

  • Raia wa Kanada, mwanasayansi wa masuala ya hali ya hewa, Profesa Katharine Hayhoe ndiye mshindi wa Tuzo la Bingwa wa Dunia lilnalotolewa na Umoja wa Mataifa, katika kitengo cha sayansi na ubunifu.
  • Ametuzwa kutokana na ujuzi wake na kwa kupenda kuangazia masuala ya mabadiliko ya tabianchi.

 

 

Septemba 16,  2019 --Raia wa Kanada, mwanasayansi wa masuala ya hali ya anga, Profesa Katharine Hayhoe ndiye mshindi wa Tuzo la Bingwa wa Dunia mwaka wa 2019. Amepokea tuzo la kiwango cha juu sana linalotolewa na Umoja wa Mataifa kutokana na juhudi zake za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na juhudi zake za kipekee za kusaidia kubadilisha mielekeo ya watu. 

 

Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) lilimtuza Hayhoe katika kitengo cha sayansi na ubunifu.

 

Hayhoe ni profesa katika Idara ya Sayansi ya Siasa katika Chuo Kikuu cha Texas Tech na nimkurugenzi wa Kituo cha Hali ya Hewa. Utafiti wake umekuwa na manufaa kwa uundaji wa sera Marekani katika majimbo na katika serikali za mitaa nchini Marekani na kwengineko. 

 

Pia, ni mmojawapo wa washawishi wakubwa duniani wanaozungumzia hali halisi ya mabadiliko ya tabianchi na anaheshimiwa mno kutokana na uwezo wake wa kuelimisha watu zaidi kuhusu wanayafahamu na kuwaonyesha madhara watakayokumbana nayo kutokana na mabadiliko ya tabianchi. 

 

Hayhoe ni mwandishi mkuu wa ripoti nyingi muhimu zinazohusu mazingira, ikiwa ni pamoja na ripoti ya Marekani ya ‘US Global Change Research Program’s Second, Third, and Fourth National Climate Assessments'. Pia, amefanya uchunguzi kuhusu mabadiliko ya tabianchi katika miji na kanda na kuwawezesha wadau kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa chakula, maji na miundo mbinu na kuonyesha umuhimu wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika ngazi ya kitaifa na kikanda.

 

"Profesa Katharine Hayhoe amejitolea maishani mwake kufanya utafiti kuhusu athari za mabadiliko ya tabianchi na kueneza matokeo ya tafiti zake mbali iwezekanavyo ili kuchochea waunda sera na wananchi kuchukua hatua,"  alisema Inger Andersen, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa.

 

"Tunapoongeza juhudi zetu mara dufu ili kupunguza athari mbaya zaidi za mabadiliko ya tabianchi, tunahitaji watu wa kujitolea sana, wanaosababisha mabadiliko kutokana na elimu walio nayo watuongoze jinsi tunavyoweza kuwa na siku zijazo endelevu. Kwa kuwa mtaalamu asiyechoka, Profesa  Hayhoe anatuongoza huku tukimfuata." Andersen alisema.

 

Wakati wa Mkutano Mkuu wa Kushughulikia Mazingira wa Umoja wa Mataifa utakaofanyika tahere 23 Septemba katika mji wa New York, Suala la umuhimu wa kuchukua hatua kali ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi litaangaziwa. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito kwa viongozi duniani, wamiliki wa biashara na mashirika ya uraia kuhudhuria mkutano wakiwa na suluhisho jinsi watakavyopunguza uchafuzi wa hewa kwa asilimia 45 kufikia karne ijayo na kuepukana na hewa chafu kabisa kufikia mwaka wa 2050. Hii ni sambamba na Makubaliano ya Paris kuhusu  tabianchi na Malengo ya Maendeleo Endelevu. 

 

Hayhoe, ambaye ni mke wa mchungaji ambaye pia huandika vitabu Andrew Farley, ni mshindi wa matuzo kadhaa kutokana na kazi yake. Mojawapo ya matuzo hayo ni Tuzo la nane la 'Stephen H. Schneider Award for Outstanding Climate Science Communication' katika mwaka wa 2018. Pia, alitambuliwa na gazeti la TIME's kam mmojawapo wa watu waliokuwa na ushawishi mkubwa katika mwaka wa 2014. Pia alitambuliwa mara pili kama 'Foreign Policy’s 100 Global Thinkers', mwaka wa 2014 na mwaka wa 2019.

 

"Nina furaha isiyokuwa na kifani kutuzwa na Umoja wa Mataifa," alisema Hayhoe, ambaye pia alitambuliwa na FORTUNE kama mmojawapo wa viongozi 50 waliojitolea zaidi. Pia alipokea tuzo la ‘Sierra Club’s Distinguished Service award’. 

 

"Tuzo hili linatutia moyo wa kuendelea kufanya kazi yetu ya kila siku ya kusambaza ujumbe kuhusu uhalisia wa mabadiliko ya tabianchi na tunapaswa kuchukua hatua za kukuabiliana nayo. Tukishirikiana, licha ya shinikisho, tutafaulu kwa sababu tayari tuna teknolojia na maarifa ya kuleta mabadiliko yanayohitajika. Kinachokosekana tu ni kujitolea,"alisema Hayhoe.

Mabingwa wa Dunia, ni tuzo la kimataifa linalotolewa na Umoja wa Maataifa kwa heshima ya mazingira. Lilianzishwa na UNEP mwaka wa 2005 kuwatuza watu wa kipekee ambao matendo yao yamekuwa na athari chanya zinazoleta mabadiliko kwa mazingira. Kutoka kwa viongozi duniani hadi kwa watetezi wa mazingira na hadi kwa wanaobuni teknolojia, waanzilishi hawa wanaleta mabadiliko ili kutunza sayari yetu kwa ajili ya vizazi vijavyo.

 

Hayhoe ni mmoja wa washindi wa huu mwaka. Vitengo vingine ni pamoja na Uongozi wa sera , motisha na kuchukua hatua  na sayansi na ubunifu  Washindi wa mwaka wa 2019 watatuzwa wakati wa sherehe ya gala mjini New York tarehe 26 Septemba wakati wa kikao cha 74 cha Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Wengine watakaotuzwa pia wakati wa tukio hili ni wanamazingira wa kipekee saba wa umri wa kati ya miaka 18 hadi miaka 30. Watatuzwa tuzo la Vijana Bingwa Duniani. 

 

Watu waliowahi kushinda tuzo la Mabingwa wa Dunia katika kitengo cha sayansi na na ubunifu ni pamoja na Impossible Foods na Beyond Meat katika mwaka wa 2018 kwa kutengeneza baga mbadala badala ya baga za nyama; Mwanamtindo kutoka Australia Leyla Acaroglu ni mshindi wa mwaka wa 2016 kwa kazi yake endelevu; na mwanakemia wa masuala ya anga Sir Robert Watson ni mshindi wa mwaka wa 2014.

 

MAKALA KWA WAHARIRI

 

Kuhusu Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa

UNEP ni msemaji mkubwa wa kimataifa kuhusu mazingira. Hutoa uongozi na kuhimiza ushirikiano katika kutunza mazingira kupitia kuvutia, kuelimisha na kuwezesha mataifa na watu kuimarisha maisha yao bila kuhatarisha yale ya vizazi vijavyo.  

 

Kuhusu Weibo

Mabingwa wa Dunia huandaliwa kwa msaada wa ufadhili kutoka kwa Weibo-Mtandao mkuu wa kijamii nchini China unaowezesha watu kuunda, kushiriki na kupata makala mtandaoni. Weibo ina zaidi ya watumizi 486 kila mwezi. www.weibo.com

 

Kuhusu Mabingwa wa Dunia

Tuzo linalotelewa kila mwaka la Mabingwa wa Dunia, hutuza viongozi vya kipekee kutoka kwa serikali, mashirika ya uraia na sekta ya kibinafsi ambao matendo yao yamesababisha mabadiliko chanya kwa mazingira. Tangu mwaka wa 2005, tuzo la Mabingwa wa Dunia limewatuza washindi 88, kuanzia kwa wakuu wa nchi hadi kwa wanaobuni teknolojia .  Tembelea tovuti.

 

Kwa maelezo zaidi, tafadhali wasiliana na:

Keisha Rukikaire, UNEP News & Media, rukikaire@un.org, +254 722 677747

Nyoka aina ya the black mamba ina sumu mbaya zaidi katika eneo la Kusini mwa jangwa la Afrika. Ukiumwa mara moja unaweza kupoteza maisha yako ndani ya masaa machache. Pia ndilo jina linalotumiwa na kitengo cha kukabiliana na uwindaji haramu kinachojumuisha wanawake tu kinachofanya kazi katika Hifadhi ya Asili ya Balule, hifadhi ya kibinafsi katika heka 56,000 katika Mbuga ya Kitaifa ya Kruger nchini Afrika Kusini.

Jina lililochaguliwa linawakilisha "nguvu walizonazo Mamba, na madhara yanatokea kwa haraka," alisema Valeria van der Westhuizen, meneja wa mawasiliano wa kikundi cha Mamba. "Nguvu za wanawake Afrika Kusini, ni nguvu za Mamba."

Kikundi cha Black Mambas kilianzishwa mwaka wa 2013 na kinajumuisha wanawake 14, wengi wao wakitoka katika jamii ya Phalaborwa inayoishi karibu na mbuga hiyo. Kabla ya kikundi hiki kuundwa, uwindaji haramu ili kupata pembe za vifaru na nyama ya wanyama mwitu lilikuwa ni jambo la kawaida, huku wawindaji haramu- wengi wao kutoka kwa jamii ya wenyeji- walipata dola za Marekani 26,000 kwa mauzo ya pembe moja. Leitah Mkhabela, msimazi wa kikundi cha Mamba, alisema kuwa sababu iliyofanya wanajamii wanaoishi karibu na mbuga kutojitolea ilitokana na sababu kuwa hawakuhisi kuwa na uhusiano na wanyama pori. Hii ni kwa sababu wengine wao hawajawahi kuona wanyama pori. Uwindaji haramu ilikuwa njia ya kutengeneza pesa nyingi, kwa haraka.

Hii ndiyo sababu mojawapo wa kazi ya kikundu cha Mamba ni kuelimisha kuhusu umuhimu wa kuhifadhi na kukusanya taarifa kutoka kwa wenyeji kuhusu wawindaji haramu.

"Jamii inapaswa kunufaika kutokana na mbuga zilizoko karibu," alisema Mkhabela, huku akionyesha majadiliano yanayoendelea kote barani Afrika kuhusu maeneo yaliyohifadhiwa. "Iwapo mbuga za wanyama zinaweza kuzinufaisha jamii za wenyeji kwa kuzipa vyanzo vya maji safi au kutoa ufadhili kwa elimu ya ngazi za juu, tutashuhudia upunguaji wa uwindaji haramu wa vifaru na wa kupata nyama ya wanyama pori."

Kupitia Programu ya Kuelimisha kuhusu Mazingira ya Wana wa Misitu (Bush Babies Environmental Education Program), haswa kwa watoto kutoka kwa jamii zilizo karibu na mbuga ili waone wanyama. "Kuna baadhi ya watu ambao wanaishi kilomita 10 tu kutoka kwenye mbuga, lakini hawajawahi ona kifaru, simba na tembo katika maisha yao," alisema Mkhabela.

Kando na kuelimisha jamii za wenyeji, kikundi cha the Black Mambas huchunga kilomita 126 za mpaka wa mbuga hiyo killa siku, huku wakitafuta mitego, kukagua ua unaotumia umeme, na kukagua magari. Kazi yao imepunguza uwindaji haramu katika mbuga hiyo kwa asili mia 75.

"Katika mwaka wa 2013, wakati mradi huu ulipoanzishwa, tulikuwa tunapata mitego mipya 80 iliyowekwa baada ya ukaguzi, alisema Mkhabela. "Sasa tunapokagua eneo lote tunaweza kurudi tu na mitego mitano, baadhi yake ikiwa kuukuu.

Cecilia Njenga, mkuu wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa katika eneo la Afrika Kusini alisema kuwa kikundi cha the Black Mambas kilionyesha wazi umuhimu na mafanikio ya elimu kwa wenyeji na kujitolea kwao ni muhimu kukabiliana na biashara haramu ya wanyama pori.

Kikundi cha the Black Mambas kinatoa motisha, siyo tu kwa wenyeji, bali kote ulimwenguni kwa wote wanaofanya kazi ili kukomesha janga ya biashara haramu ya wanyama pori," alisema Njenga. "Tunatambua mafanikio ya kasi na ya kupendeza walioyapata, na ushupavu unaohitajika kuyafikia.

image
Picha na Julia Gunther

Ijapokuwa hakuna chochote kilicho na umuhimu kuliko utunzaji wa wanyama pori, Mkhabela anasema kazi hii siyo ya kila mtu. Kutokana na mishahara duni, ya takribani dola 224 za Marekani kila mwezi, mazingira mabaya ya kufanyia kazi, na hatari ya kila mara kutoka kwa wawindaji haramu, unahitaji kuwa shupavu ili kuwa askari pori.

"Mimi huhatarisha maisha yangu kila siku, ili kuhakikisha wanyama pori wa kipekee wa Afrika Kusini wako salama," alisema Mkhabela.

Kwa mfano, katika mwaka wa 2017, Mkhabela na wenzake wawili kutoka kwa kikundi cha the Black Mambas walikuwa wanavizia wawindaji haramu katika eneo la Balule, wakati ambapo wawindaji haramu, waliokuwa wanawafuata, walipowaona kutokana na nuru ya mwezi mzima jioni hiyo. Wanawake hao-ambo hupiga doria bila kuwa na sila-walibahatika kuhepa bila majeraha baada ya kupata sehemu ya ua la mbuga iliyoharibiwa, ambayo ilikuwa imetumiwa kumwondoa tembo siku hiyo.

Ila kwa mjibu wa Mkhabela hali ya kuhatarisha maisha yao ina manufaa. Alisema kuwa kwa kuwa wao ni wanawake na kina mama, kikundi cha the Black Mambas kinaelewa ni nini maana ya ya kulea na kutunza.

"Tunastahili kuzungumza kwa niaba ya wanyama kwa sababu iwapo hatutafanya hivyo, hakuna atakayezungumza kwa niaba yao. Ni sharti tupiganie maslahi yao, kwa sababu iwapo hatutafanya hivyo, hakuna atakayepigania masilahi yao. "Tunafahamu mapenzi ni nini," alisema.

image
Picha na Kate Thompson-Gorry

Katika mwaka wa 2015, Kikundi cha the Black Mambas kilitunukiwa Tuzo la Bingwa wa Dunia la Shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa kutana na mafanikio yao ya kudumu. Tangu waliposhinda, Mkhabela anasema kuwa kitengo cha kukabiliana na wawindaji haramu kimevutia watu wengi kutoka kwa jamii, kinyume na hali ya hapo awali, na hali hii imefanya kikundi cha Mambas kudhamini mno kazi yao.

Mkhabela anasema kuwa kuna wanawake wengine 10 ambao sasa hivi wanapokea mafunzo ya kujiunga na kikundi cha the Black Mambas na ana matumaini kuwa mradi wao utaendelea kuimarika na kupokea ufadhili.

"Ningependa kuona wasichana zaidi kutoka kwa jamii wakipata kazi kama askari pori," alisema. "Tunataka mradi wa the Black Mambas uendelee. "Hatuwezi kuwacha wawindaji haramu washinde."

 

Siku ya Askari Pori Duniani, mradi wa Shirikisho la Kimataifa la Askari Pori , itakuwa tarehe 31 Julai ili kusherehekea kazi wanayoifanya askari pori ili kulinda bayoanuai ya sayari na kuwakumbuka waliofariki wakifanya kazi yao.

Nyoka aina ya the black mamba ina sumu mbaya zaidi katika eneo la Kusini mwa jangwa la Afrika. Ukiumwa mara moja unaweza kupoteza maisha yako ndani ya masaa machache. Pia ndilo jina linalotumiwa na kitengo cha kukabiliana na uwindaji haramu kinachojumuisha wanawake tu kinachofanya kazi katika Hifadhi ya Asili ya Balule, hifadhi ya kibinafsi katika heka 56,000 katika Mbuga ya Kitaifa ya Kruger nchini Afrika Kusini.

Jina lililochaguliwa linawakilisha "nguvu walizonazo Mamba, na madhara yanatokea kwa haraka," alisema Valeria van der Westhuizen, meneja wa mawasiliano wa kikundi cha Mamba. "Nguvu za wanawake Afrika Kusini, ni nguvu za Mamba."

Kikundi cha Black Mambas kilianzishwa mwaka wa 2013 na kinajumuisha wanawake 14, wengi wao wakitoka katika jamii ya Phalaborwa inayoishi karibu na mbuga hiyo. Kabla ya kikundi hiki kuundwa, uwindaji haramu ili kupata pembe za vifaru na nyama ya wanyama mwitu lilikuwa ni jambo la kawaida, huku wawindaji haramu- wengi wao kutoka kwa jamii ya wenyeji- walipata dola za Marekani 26,000 kwa mauzo ya pembe moja. Leitah Mkhabela, msimazi wa kikundi cha Mamba, alisema kuwa sababu iliyofanya wanajamii wanaoishi karibu na mbuga kutojitolea ilitokana na sababu kuwa hawakuhisi kuwa na uhusiano na wanyama pori. Hii ni kwa sababu wengine wao hawajawahi kuona wanyama pori. Uwindaji haramu ilikuwa njia ya kutengeneza pesa nyingi, kwa haraka.

Hii ndiyo sababu mojawapo wa kazi ya kikundu cha Mamba ni kuelimisha kuhusu umuhimu wa kuhifadhi na kukusanya taarifa kutoka kwa wenyeji kuhusu wawindaji haramu.

"Jamii inapaswa kunufaika kutokana na mbuga zilizoko karibu," alisema Mkhabela, huku akionyesha majadiliano yanayoendelea kote barani Afrika kuhusu maeneo yaliyohifadhiwa. "Iwapo mbuga za wanyama zinaweza kuzinufaisha jamii za wenyeji kwa kuzipa vyanzo vya maji safi au kutoa ufadhili kwa elimu ya ngazi za juu, tutashuhudia upunguaji wa uwindaji haramu wa vifaru na wa kupata nyama ya wanyama pori."

Kupitia Programu ya Kuelimisha kuhusu Mazingira ya Wana wa Misitu (Bush Babies Environmental Education Program), haswa kwa watoto kutoka kwa jamii zilizo karibu na mbuga ili waone wanyama. "Kuna baadhi ya watu ambao

wanaishi kilomita 10 tu kutoka kwenye mbuga, lakini hawajawahi ona kifaru, simba na tembo katika maisha yao," alisema Mkhabela.

Kando na kuelimisha jamii za wenyeji, kikundi cha the Black Mambas huchunga kilomita 126 za mpaka wa mbuga hiyo killa siku, huku wakitafuta mitego, kukagua ua unaotumia umeme, na kukagua magari. Kazi yao imepunguza uwindaji haramu katika mbuga hiyo kwa asili mia 75.

"Katika mwaka wa 2013, wakati mradi huu ulipoanzishwa, tulikuwa tunapata mitego mipya 80 iliyowekwa baada ya ukaguzi, alisema Mkhabela. "Sasa tunapokagua eneo lote tunaweza kurudi tu na mitego mitano, baadhi yake ikiwa kuukuu.

Cecilia Njenga, mkuu wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa katika eneo la Afrika Kusini alisema kuwa kikundi cha the Black Mambas kilionyesha wazi umuhimu na mafanikio ya elimu kwa wenyeji na kujitolea kwao ni muhimu kukabiliana na biashara haramu ya wanyama pori.

Kikundi cha the Black Mambas kinatoa motisha, siyo tu kwa wenyeji, bali kote ulimwenguni kwa wote wanaofanya kazi ili kukomesha janga ya biashara haramu ya wanyama pori," alisema Njenga. "Tunatambua mafanikio ya kasi na ya kupendeza walioyapata, na ushupavu unaohitajika kuyafikia.

image
Picha na Julia Gunther

Ijapokuwa hakuna chochote kilicho na umuhimu kuliko utunzaji wa wanyama pori, Mkhabela anasema kazi hii siyo ya kila mtu. Kutokana na mishahara duni, ya takribani dola 224 za Marekani kila mwezi, mazingira mabaya ya kufanyia kazi, na hatari ya kila mara kutoka kwa wawindaji haramu, unahitaji kuwa shupavu ili kuwa askari pori.

"Mimi huhatarisha maisha yangu kila siku, ili kuhakikisha wanyama pori wa kipekee wa Afrika Kusini wako salama," alisema Mkhabela.

Kwa mfano, katika mwaka wa 2017, Mkhabela na wenzake wawili kutoka kwa kikundi cha the Black Mambas walikuwa wanavizia wawindaji haramu katika eneo la Balule, wakati ambapo wawindaji haramu, waliokuwa wanawafuata, walipowaona kutokana na nuru ya mwezi mzima jioni hiyo. Wanawake hao-ambo hupiga doria bila kuwa na sila-walibahatika kuhepa bila majeraha baada ya kupata sehemu ya ua la mbuga iliyoharibiwa, ambayo ilikuwa imetumiwa kumwondoa tembo siku hiyo.

 

image
Picha na Kate Thompson-Gorry

Ila kwa mjibu wa Mkhabela hali ya kuhatarisha maisha yao ina manufaa. Alisema kuwa kwa kuwa wao ni wanawake na kina mama, kikundi cha the Black Mambas kinaelewa ni nini maana ya ya kulea na kutunza.

"Tunastahili kuzungumza kwa niaba ya wanyama kwa sababu iwapo hatutafanya hivyo, hakuna atakayezungumza kwa niaba yao. Ni sharti tupiganie maslahi yao, kwa sababu iwapo hatutafanya hivyo, hakuna atakayepigania masilahi yao. "Tunafahamu mapenzi ni nini," alisema.

Kupitia kwa ushirikiano, tunaweza kutunza mazingira. Haya ndiyo watu wa kiasili wa Kalinga nchini Ufilipino walidhibitishia ulimwengu walipoweza kukomesha Mradi wa ujenzi wa Bwawa kwa Mto Chico. Hali hii ndiyo iliyomtia motisha Joan Carling kujitolea milele kupigania haki za binadamu wakati wa kufanya maendeleo kwenye ardhi.

"Kutokana na kanuni zilezile wanazozitumia watu wa kiasili inamaanisha kuwa tunapaswa kukuza mahusianoo yetu yanayotegemeana na mazingira ambayo ndiyo chanzo chetu," anasema Carlin anayetoka katika kabila la Kankanaey nchini Ufilipino. "Uhusiano huo ndio ninaoamini kwamba unadhalalishwa kutokana na dhana ya kimagharibi ya maendeleo."

Carling, mwenye umri wa miaka 55, alianza kazi yake kama mhamasishaji zaidi ya miaka ishirini iliyopita katika eneo la Cordillera, linalopatikana kazikazini mwa Ufilipino. Eneo hilo, ambalo ni makao ya watu milioni 1.3 wa kiasili, linapatikana sehemu ya nchi iliyo na madini mengi-kuna dhahabu, shaba na manganizi.

Sheria ya Mwaka wa 1995 ya Uchimbaji wa Madini iliruhusu mashirika ya kimataifa kumiliki mashamba yote yalio na utajiri wa madini ikiwa ni pamoja na kuwa na haki miliki kwa maji yote na mbao. Pia walipewa ruhusa ya kuwatimua wanajamii kutoka kwa maeneo yaliyoidhinishwa.

image

Joan Carling. Picha kutoka maktaba ya UN

Kwa hivyo Carling, akishirikiana na wenzake kutoka Muungano wa Cordillera People's Alliance, walianza kukusanya ujumbe kuhusu athari za uchimbaji wa madini ili kupata ushahidi wa kutumiwa ili kutoa wito kwa serikali. Anasema kuwa sababu iliyofanikisha muungano wao kufaulu kukomesha baadhi ya miradi iliyokuwa imepangwa kufanywa, ni kutokana na ushahidi iliathiri mazingira asilia, kama vile kuchafua mito kwa kemikali. Baada ya wazee kutoka katika mikoa yote kutia sahihi mkataba wa umoja ambao ulipinga kuwepo kwa kampuni za kuchimba madini, gavana wa mkoa pia aliapa kuweka sera ya kutoruhusu shughuli za uchimbaji wa madini katika wilaya yake.

"Ni wazi kuwa iwapo watu waliopo nyanjani hawatachukua hatua, wanasasia hatawajibika," alisema Carling.

Carling-kama watangulizi wake wa kiasili-ametoa kauli za kupinga ujenzi wa mabwawa. Ijapokuwa anatambua kuwa watu wengi huchukulia mabwawa kama chanzo cha nishati jadidifu, anasema kuwa mbali na kuharibu ekolojia nyingi za mito kote ulimwenguni, pia yamesabasha watu kupoteza makazi yao.

Utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na chuo kikuu cha Sussex na Shule ya Kimataifa ya Menejimenti nchini Ujerumani uligundua kuwa nchi zinazotegemea nishati ya maji sanasana kutoka kwa mabwawa ili kupata umeme yana viwango vikubwa vya umaskini, ufisadi na madeni ikilinganishwa na nchi nyinginezo.

"Ni wazi kuwa mabwawa hupendelewa kwa sababu ya faida kubwa wanayopata wajengaji wa mabwawa, fursa kubwa kwa viongozi wafisadi kunenepesha mifuko yao. Faida hiyo ndiyo inaendesha biashiara ya mabwawa, kushinda kuhitajika kwake," alisema.

image

Chimbo la Shaba Ufilipino Picha na Wikicommons

Pia, nchi nyingi zinazoendelea, huchukulia ujenzi wa mabwawa kama kitu kinacholeta maendeleo ya uchumi kwa haraka. Carling analifahamu hili, na ndiyo sababu hapingi kabisa kuwepo kwa miradi ya mabwawa, lakini "kuwe na mbinu inayozingatia haki za binadamu wakati wa maendeleo ya kuleta nishati".

"Watu wa kiasili siyo maadui. Hatupingi maendeleo," alisema. "Lakini mojawapo wa mapendekezo makubwa yalitolewa na Kamisheni ya Mabwawa Duniani ni nchi kufanya uchunguzi wa njia mbadala kwa kuzingatia kuhitajika kwa nishati. Kuna njia mbalimbali, siyo mabwawa tu."

Na hii ndiyo sababu Carling anachunguza matumizi ya mbinu zinginezo: ubia na sekta za kibinafsi. Anatumai kuwa kwa kushirikiana na wanaopigania mazingira wakati wa biashara, inaweza kusaidia kuonyesha uwezekano wa kuwa na maendeleo endelevu.

Carling aliatunukiwa tuzo la Mabingwa wa Dunia linalotolewa na Shirka la Mazingira la umoja wa Mataifa kwa mafanikio yake ya kudumu mwaka wa 2018.

Leyla Acaroglu alikuwa na umri wa miaka 19 wakati wake wa kwanza kuhudhuria somo la kubuni michoro. Alisikia kitu ambacho kilibadili mtazamo wake kuhusu dunia milele.

Prof aliyemfundisha kubuni michoro alikuwa anafunza kuhusu nadhariatete ya Gaia: nadharia inayoshikilia kuwa kila kitu ulimwenguni kina uhusiano na kingine. Kama watu wa kubuni michoro, aliwasisitizia, kuna uwezekano kuwa siku moja watafanya maamuzi ambayo yatakuwa na athari kubwa mno kwa mazingira bila hata wao wenyewe kutambua.

"Niliketi pale huku nikiitazama picha ya tsunami na kuwaza 'Vipi! Kwa nini hakuna aliyenifahamisha kuhusu suala hili? Mbona ni mara ya kwanza kujifunza kuhusu swala hili?'," alisema Acaroglu.

"Siwezi kueleza jinsi nilivyohisi," alisema. Kwa hivyo, Acaroglu aliamua maishani  mwake analenga kubuni michoro endelevu na kuwasaidia watu kutengeneza bidhaa bora na kutoa huduma zitakazokuwa na madhara machache kwa mazingira.

Leo hii, Acaroglu ni mshindi wa Tuzo la Bingwa wa Dunia linalotolewa na Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa kutokana na juhudi zake za kueneza michoro yenye suhuhu endelevu. Ana imani ya dhati kuwa tuko katikati ya kipindi cha mabadiliko ya kitamaduni kuelekea uchumi unategemea nishati jadidifu kutokana na ukosefu wa mbinu mbadala za kutumia katika sayari yetu.

“Kuna changamoto ya kiubunifu itakayotuwezesha kubadilisha jinsi tunavyofanya mambo. Kubuni michoro siyo tu kubuni kiti kizuri sana, kubuni michoro ni kuchukua rasilimali yoyote na kuunda kitu kipya," alisema. "Tunajiandaa kutofaulu iwapo hatutajitokeza na mfumo unaotegemea nishati jadidifu.” 

image

Acaroglu, mwenye umri wa miaka 36 na mwanzilishi wa vituo viwili vya kubuni michoro—mojawapo kinashughulikia hali zinawezesha kampuni kupokea mafunzo ya kuziwezesha kutumia nishati jadidifu—anasema kuwa mifumo mingi ya biashara inayorurusiwa na serikali kubuniwa ni "isiyoweza kubadilika."

"Hatuna sera zinazounga mkono aina ya ubunifu unaotumia njia anuai katika jamii. Ni nchi chache tu ulimwenguni zinazoruhusu hili kutokea," alisema.

Falsafa yake ni kuwa badala ya kuuza tu bidhaa, ambavyo ni kazi ya mtumiaji kuvitupa akimaliza kutumia, kampuni ni sharti ziunde bidhaa vya misimu yote, vinavyoweza kutumiwa tena na vyenye manufaa ya kiuchumi kutokana na uwezo wa kutumika tena, tangu mwanzo.

Acaroglu anasema njia mwafaka ya kuchunguza madhara ya bidhaa kwa mazingira ni kutathmini mda wa matumizi yake kabla ya kuharibika, kwa sababu inaangalia athari ya vitu vinayoathiri uchumi tangu kutengenezwa hadi kutumika kwake.

Mbali na kutoa mafunzo kwa kampuni, pia ameunda thecircularclassroom.com kuwasaidia wanafunzi kufikiri tangu wakiwa na umri mdogo kuhusa bidhaa zinazoweza kutumiwa tena na wala si za matumizi ya mara moja. Aliundia nchi ya Ufini mtaala na sasa hivi anaundia nchi ya Thailandi mfumo mzima wa kufunzia, utakaotumika kando na ule utumikao shuleni.

"Mfumo wetu mbaya wa elimu haujengei vijana uwezo wa yale wanaohitaji kubuni uchumi mpya tunaouelekea," alisema.

Anasema yeye ni ashiki mkubwa wa Buckminster Fuller—wa maono ya siku za usoni aliyekuwa maarufu miaka ya 1950 kwa kubuni 'geodesic dome'—Acaroglu alisema kulichomvutia zaidi na Fuller ni uwezo aliokuwa nao wa kuathiri watu kuhusu mambo ya siku zijazo na jinsi ya kuleta mabadiliko ulimwenguni.

"Tunaishi kwa hali isiyoeleweka," alisema. "Hakuna chochote kinachoweza kutupa motisha katika hii dunia. Tunao uwezo wa kuharibu au kubuni katika hali hii."

Mabingwa wa Dunia, tuko kuu linalotolewa na Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa, huwatambua watu mashuhuri kutoka kwa sekta na umma na za kibinafsi, na kutoka kwa mashirika ya uraia ambao kazi zao zimeleta mabadiliko chanya kwa mazingira. Iwapo unamfahamu mtu wa aina hii, mchague ili awe Bingwa wetu anayefuata.

Video

Paul A. Newman na Kituo cha NASA’s Goddard Space Flight Center ni Bingwa wa Dunia wa mwaka wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa katika kitengo cha Sayansi na Ubunifu na kutokana na mchango wao wa kipekee kwa Mkataba wa Montreal- ambao umepunguza vitu vinavyoharibu ozoni kwa asili mia 99 na kusababisha tambiko la ozoni kuboreka.

Video

Katika video hii fupi, tazama wakati muhimu kabisa wa Maonyesho ya Tuzo la Mabingwa wa Dunia la Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa yalioendeshwa na Dia Mirza na Alec Baldwin na yaliyofanyika Septemba 26, 2018 katika mji wa New York City.

Video

Michelle Bachelet, Rais wa Chile, ni Bingwa wa Dunia wa mwaka wa 2017 kutokana na uongozi wake wa kipekee wa kuunda maeneo ya bahari yaliyohifadhiwa na kukuza nishati jadidifu.

Video

Mshindi wa tuzo la utengenezaji filamu, Jeff Orlowski, ni Bingwa wa Dunia wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa kutokana na mafanikio yake ya kutuma jumbe nzito kuhusiana na mazingira kwa watazamaji kote ulimwenguni.