Video

Wang Wenbiao, Mwenyekiti wa Kikundi cha Elion Resources Group ni Bingwa wa Dunia wa mwaka wa 2017 kutokana na mafanikio yake ya kudumu.

Video

Jamii ya upandaji miti ya Saihanba, ni Bingwa wa Dunia wa mwaka wa 2017 wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa kutokana na kufanya ardhi iliyoharibika kuzalisha miti mingi.

Video

Paul A. Newman na Kituo cha NASA’s Goddard Space Flight Center ni Bingwa wa Dunia wa mwaka wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa katika kitengo cha Sayansi na Ubunifu na kutokana na mchango wao wa kipekee kwa Mkataba wa Montreal- ambao umepunguza vitu vinavyoharibu ozoni kwa asili mia 99 na kusababisha tambiko la ozoni kuboreka.

Thank you for subscribing.

Kutoka kwa washindi kutoka nyanjani na viongozi wa taasisi hadi kwa wanasiasa wa kipekee na taasisi za utafiti, UNEP inasherehekea Washindi wanaofanya maamuzi ya kipekee kwa manufaa ya dunia yetu. 

Tangu kuanzishwa kwake mwaka wa 2005, tuzo la Mabingwa wa Dunia linalotolewa na Umoja wa Mataifa ni tuzo la ngazi ya juu linalotolewa kwa heshima ya mazingira. 

Kila mwaka, UNEP hutuza watu binafsi na mashirika yanayofanya kazi kupata masuluhisho bunifu na endelevu ya kushughulikia changamoto za aina tatu duniani za mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa mazingira na bayoanuai, na kemikali, uchafuzi na taka. Mabingwa hubadilisha uchumi wetu, huvumbua, huongoza mabadiliko ya kisiasa, hupambana na ukosefu wa haki ya mazingira na kupigania malighafi zetu. 

Mabingwa wa Dunia huwatuza watu katika vitengo vinne:

  • Uongozi unaozingatia sera Maafisa wa sekta ya umma wanaoongoza hatua za kimataifa au kitaifa za kushughulikia mazingira. Wao huendeleza mijadiliano, kujitolea kwa dhati na kuchukua kwa manufaa ya sayari.
  • Motisha na kuchukua hatua Viongozi wanaochukua hatua madhubuti zinazopelekea mabadiliko chanya ya kutunza dunia yetu. Maongozi yao ni ya kupigiwa mfano, wanatuhimiza kubadilisha mienendo yetu na kutia moyo mamilioni ya watu.
  • Maono ya ujasiriamali Watu walio na maono ya kipekee yanayoenda kinyume na hali ya kawaida ya kukuza mustakabali usiochafua mazingira. Wao hukuza mifumo, kubuni teknojia mpya na kujitokeza na maono mapya ya kipekee.  
  • Sayansi na ubunifu Waanzilishi wanaotumia teknolojia kikamilifu kwa manufaa makuu ya mazingira. Ubunifu wao unaweza kupelekea kuwepo na siku za usoni endelevu.

Tuzo la Mabingwa wa Dunia limewatuza washindi 116, ikijumuisha viongozi duniani na watu wanaobuni teknolojia. Wanajumuisha Viongozi wa dunia 27, watu binafsi 70 na makundi au mashirika 19. 

2019 Champions of the Earth award ceremony. Photo: UNEP

 

Tuzo la Mabingwa wa Dunia hutuza watu binafsi na mashirika ambayo huchukua hatua za kusababisha mabadiliko chanya kwa mazingira. 

UNEP inatafuta kupendekezwa kwa watu binafsi na mashirika yanayofanya kazi kupata masuluhisho bunifu na endelevu ya kuboresha ardhi, kuimarisha ustahimilivu kwa ukame, na kupambana na kuenea kwa majangwa. 

Upendekezaji wa wawaniaji wa awamu ya mwaka wa 2024 unaendelea kwa sasa

.

Upendekezaji unaweza kufanywa katika viwango vinne

Mchakato wa kuchaguliwa

Wafanyakazi wa UNEP na wataalam wa mada husika huchagua kutoka kwa orodha ya mapendekezo yaliyopokelewa kutoka kote duniani. Mtu yeyote anaweza kutoa mapendekezo/kupendekezwa. Katika mwaka wa 2023, UNEP ilipokea mapendekezo 2,500, na kuwa mwaka wa tatu mfululizo wa kupokea mapendekezo mengi zaidi.  

Vigezo vya kuchaguliwa ni kama vifuatavyo:

  • Athari: Je, juhudi za aliyependekwa zimepelekea manufaa makubwa ya kimazingira au zimeonyesha kuwa na uwezekano mkubwa wa kurudufishwa na kuimarishwa zaidi?
  • Mambo mapya: Je, aliyependekezwa amefanya au kupelekea kitu kipya na bunifu?   
  • Ushawishi:  Kisa cha aliyependekezwa kinavutia kwa kiwango kipi?

 

Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa hujivunia kufanya kazi na wabia kutambua na kusherehekea mafanikio ya kipekee ya washindi wa tuzo la Mabingwa wa Dunia.

Ni kutokana na ukarimu wao mkuu ndipo tunapoweza kuendelea kusherehekea mafanikio yao. Wabia wetu hufadhili juhudi za Mabingwa wa Dunia na Vijana Bingwa Duniani.

Weibo

Weibo imejitolea kuimarisha juhudi za kushughulikia utunzaji wa mazingira na maendeleo endelevu. Tayari imefadhili kampeni kadhaa za Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa kwa mitandao yake katika miaka ya hivi karibuni, ikiwa ni pamoja na Siku ya Mazingira Duniani na kampeni ya Wild for Life.

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cochin ni uwanja wa ndege wa kwanza kutumia nishati ya jua duniani. Hutekeleza kazi zake zote kwa kutumia nishati ya jua. Ni uwanja wa ndege mkubwa zaidi na wenye shughuli nyingi zaidi katika jimbo la Kerala nchini India, na pia ni uwanja wa ndege wenye shughuli nyingi zaidi nchini India kwa kuzingatia mlolongo wa ndege za kimataifa. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cochin ulianza kufanya kazi kikamilifu kwa kutumia nishati ya jua mwaka wa 2015 - mradi ulioanzishwa na Mkurugenzi Mwendeshaji Vattavayalil Joseph Kurian.

Hababi David Attenborough alipokuwa mdogo, alitumia mwingi wa muda wake alipokuwa hafanyi kazi kupitia machimbo yaliyosahaulika maeneo ya mashambani nchini Uingereza huku akiwa na nyundo mkononi. Alichowinda: visukuku vilivyo na amonia, moluska wenye umbo la mzunguko walioishi wakati wa dinosaria.

Kwa Attenborough akiwa kijana, visukuku vilikuwa kama hazina iliyozikwa na alishangaa kuwa wa kwanza kuviona katika kipindi cha mamilioni ya miaka.

Ulimwengu asilia umeendelea kumfurahisha maisha yake yote.

Kwa sasa, Attenborough mwenye umri wa miaka 95, bila shaka ndiye mtangazaji anayejulikana zaidi katika historia kwa kutangaza kuhusu ulimwenguni asilia vizuri zaidi. Wakati wa kazi yake iliyoanza wakati televisheni zilipoziduliwa, ameandika na kuwasilisha baadhi ya filamu zenye ushawishi mkubwa kuhusu hali ya sayari, ikijumuisha mfululizo wa makala yake kwa kipindi cha muongo mmoja, yalio na sehemu tisa za Awamu za Maisha.

Kupitia kile New York Times ilichokiita "masimulizi kupitia sauti ya Mungu" na udadisi usiokoma, ametumia miaka 70 kufichua urembo wa ulimwengu asilia - na kufichua vitisho vinavyoukabili. Kwa kufanya hivyo, ametoa matumaini kwa mamilioni ya watazamaji ya kuwa na mustakabali endelevu.

“Ikiwa kwa kweli, ulimwengu ungeweza kuokolewa, basi Attenborough angefanya zaidi kuuokoa kuliko mtu mwingine yeyote aliyewahi kuishi,” aliandika mwanamazingira na mwandishi Simon Barnes.

Umoja wa Mataifa umetambua athari kubwa ya Attenborough kwa vuguvugu la kimataifa la mazingira, na kumkabidhi tuzo la Mabingwa wa Dunia la Umoja wa Mataifa kwa Mafanikio ya Kudumu. Tuzo hili ni tuzo la Umoja wa Mataifa la ngazi ya juu linalotolewa kwa heshima ya mazingira na linasherehekea wale waliojitolea maishani kukabiliana na majanga kama vile mabadiliko ya tabianchi, uangamiaji wa spishi na uchafuzi.

"Umekuwa mtu wa kuigwa na watu wengi," Inger Andersen, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), alipokuwa akimkabidhi Attenborough tuzo hilo.

"Ulizungumza kwa niaba ya sayari kwa muda mrefu kabla ya mtu mwingine yeyote kufanya hivyo na unaendelea kutuelekeza kuliko na hatari."

Pamoja na kazi yake katika vyombo vya habari, Attenborough ni mojawapo ya wahamasishaji wakuu wa vuguvugu la mazingira duniani. Amehudhuria mikutano mikuu ya kilele kama vile Kongamano la Mabadiliko ya Tabianchi mjini Paris Mwaka wa 2015, ambapo alitoa wito wa kuwepo na ushirikiano kote ulimwenguni kwenye juhudi za kukabiliana na vitisho kwa Dunia.

Pia ameshirikiana na UNEP kwa angalau miongo minne, akitumia sauti yake kwa mfululizo wa kampeni na filamu fupi ambazo zimeangazia juhudi za shirika hili za kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa bayoanuai na uchafuzi. Kazi hiyo inaendeshwa na imani kwamba hakuna nchi moja tu inayoweza kutatua matatizo ya mazingira duniani.

"Tunaishi katika enzi ambayo utaifa hautoshi," Attenborough alisema alipokuwa anapokea Tuzo la UNEP la Mabingwa wa Dunia kwa Mafanikio ya kudumu. "Lazima tuhisi kama sisi sote ni raia wa sayari hii moja. Tukishirikiana, tunaweza kutatua matatizo haya.”

Attenborough alihitimu kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge katika mwaka wa 1947 na shahada sayansi ya asili, lakini akabaini kuwa hageweza kufanya tu utafiti maisha yake yote. Hapo, akajiunga na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) wakati televisheni ilivyokuwa ikianza kujipenyeza majumbani.

Alionekana mara ya kwanza kwenye runinga tarehe 21 Desemba, mwaka wa1954, kwenye Zoo Quest, mfululizo wa makala yaliyopelekea Waigereza kutazama viumbe mbalimbali kutoka pembe zote za dunia kama vile orangutan na Dragoni wa Komodo.

Akiwa msimamizi mwenye kipaji kama alivyokuwa mtangazaji mwenye kipaji, Attenborough alipanda vyeo kama mtangazaji wa kitaifa wa Uingereza, na hatimaye akaja kuongoza BBC Two. Huko, alizindua Monty Python’s Flying Circus, na mfulizo wa filamu nyinginezo.

Lakini kazi ya kuwa msimamizi haikumfurahisha, na katika mwaka wa 1973 Attenborough aliachana na ofisi kuu na kurudi kuunda filamu.

Matokeo yake yalikuwa mfululizo wa filamu zake kuu Life on Earth katika mwaka wa 1979, zilizoonyesha historia ya viumbe duniani, kuanzia kwa vijidudu vya kwanza hadi kwa wanadamu.

Filamu hizo zilichukua miaka tatu kutengeneza na Attenborough alisafiri maili milioni 1.5 wakati wa utengenezaji wa filamu hizo. Kwa kuzingatia upeo na matarajio yake, Life on Earth ilibadili filamu ya masimulizi kuhusu historia ya asili na kutazamwa na watu wapatao milioni 500.

Katika miongo mitatu iliyofuata, Attenborough alitunga na kuwasilisha filamu nane bora zaidi, akielekeza ulimwengu kwa kile alichokiita “spectacular marvel” ya asili.

Lakini kazi yake iliposonga mbele, Attenborough alikuja kutoa ushahidi wa kulipuliwa kwa ulimwengu asilia. Idadi ya binadamu ilipoongezeka, asili ilipungua. Shughuli za binadamu zimebadilisha robo tatu ya eneo la Dunia na kuweka spishi milioni moja hatarini kutoweka.

"Ijapokuwa tuko imara leo, ni wazi kuwa tutakuwa imara zaidi katika siku zijazo," alisema wakati wa kuhitimisha The Living Planet katika mwaka wa 1984. "Ni wazi tunaweza kuangamiza ulimwengu. [Dunia] kuendelea kuwepo sasa iko mikononi mwetu.”

Filamu za Attenborough zilionyesha ulimwengu kuwa wanyamapori wanaweza kuangamia, kwamba ni wadhaifu na wanahitaji kulindwa - na kwamba wanadamu wanaendelea kuwa hatari kwa asili.

Mwaka jana, katikati ya miaka yake 90, alihutubia viongozi wa dunia katika Kongamao la Umoja wa Mataifa la Mabadiliko ya Tabianchi mjini Glasgow, Scotland.

“Tayari tuko hatarini,” alisema. “Je hii ndiyo hatima ya hali yetu? Hali halisi ya spishi bora zaidi zimeangamizwa kutokana na tabia ya binadamu ya kushindwa kuona hali kamili wanapokimbizana na malengo ya muda mfupi.”

Lakini basi, kama kawaida, maneno ya Attenborough yalileta matumaini. Mada inayojitokeza mara kwa mara kweye filamu zake ni kuwa licha ya hali mbaya ya sayari, binadamu bado wanaweza kupunguza madhara waliofanya.

"Hatujakata tamaa," alisema katika mwaka wa 2020 wakati wa A Life on Our Planet,, akiangazia kazi yake hapo awali. "Kuna fursa ya kuboresha mambo, kukamilisha safari yetu ya maendeleo na kwa mara nyingine tena tujali asili. Tunachohitaji ni nia ya kufanya hivyo."

Katika filamu iyo hiyo, alitoa maagizo ya kufanya amani na asili. Ilijikita katika kuinua viwango vya maisha katika nchi maskini ili kupunguza ongezeko la watu, kutumia nishati isiyochafua mazingira, kama nishati ya jua na upepo, kula vyakula vingi vinavyotokana na mimea, visivyodhuru mazingira, na kuachana na nishati ya visukuku.

"Tukitunza asili, asili itatutunza," alisema. "Sasa ni wakati wa spishi zetu kuacha kukua tu, kuishi kwenye sayari yetu kwa kujali mazingira, ili kuanza kustawi."

Kazi na uanaharakati wa Attenborough ilimpelekea kufanywa hababi (mara mbili) na jina lake kuongezwa kwa aina mbalimbali ya spishi, kuanzia kwa attenborosaurus (mtambaazi wa zamani wa kuogelea) hadi kwa nepenthes attenboroughii (mmea alaye wanyama).

Katika miaka ya hivi karibuni, Attenborough ameendelea kuandaa makala ya filamu kuhusu asili, na kujishindia matuzo mawili ya Emmy ya masimulizi katika mwaka wa 2021. (Katika kazi yake, ameshinda matuzo matatu ya Emmy na BAFTA nane.)

Kwa miongo kadhaa, Attenborough amekuwa akitafutwa na viongozi duniani wanaotafuta suluhu kwa majanga yanayokabili ulimwengu asilia - na hata pegine kutaka kuhisi kujitolea kwake.

Katika mwaka wa 2015 alizuru Ikulu ya White House kwa mazungumzo na Rais wa Marekani Barack Obama. Obama alimuuliza Attenborough ni nini kilimchochea kuanza kuwa na “kuupenda mno” ulimwengu asilia.

“Sijawahi kukutana na mtoto asiyependa historia ya asili,” alijibu, labda akikumbuka siku alipowinda visukuku vijijini Uingereza. "Kwa hivyo, swali ni, mtu anawezaje kutozigatia haya?"